Blogu hii imedhaminiwa na Simba Video Coach

Blogu hii imedhaminiwa na Simba Video Coach
Kwa usafiri wa Dar es salaam, Morogoro, Dodoma na Arusha, safiri kwa raha na Simba Mtoto Luxury Coach

Wednesday, November 30, 2011

RC-TANGA AONGOZA KIKAO CHA KWANZA CHA BODI YA BARABARA TANGA

MKUU WA MKOA WA TANGA LUTENI CHIKU GALLAWA AKIFUNGUA KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA TANGA

BAADHI YA WAJUMBE WA KIKAO CHA BODI YA BARABARA KUTOKA WILAYA YA KOROGWE WAKIONGOZWA NA DC WAKE BW. ERSTO SIMA (KATIKATI) WAKISIKILIZA KWA MAKINI UWASILISHAJI WA MADA MBALIMBALI KUHUSU BARABARA ZA MKOA WA TANGA

KAIMU MENEJA WA WAKALA WA BARABARA MKOA WA TANGA TANROADS INJINIA ALFRED NDUMBALO AKIWASILISHA TAARIFA YA UFANYAJI KAZI WA WAKALA HIYO KATIKA KIKAO CHA BODI YA BARABARA

MAOFISA WA MKOANI WAKIENDELEA NA ZOEZI LA KUREKODI ORODHA YA WAJUMBE WA KIKAO CHA BODI YA BARABARA

BAADHI YA WAJUMBE KUTOKA WILAYA YA MUHEZA MBUNGE WA JIMBO LA MUHEZA BW. HERBERT MNTANGI (kulia) NA MWENYEKITI WA HALMASHAURI HIYO BW. AMIR KIROBOTO

MAKAMO MPYA WA KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA TANGA BW. SALEH PAMBA (KUSHOTO), MWENYEKITI WA CCM MKOA WA TANGA BW. MUSSA SHEKIMWERI NA MWENYEKITI WA KIKAO CHA BODI YA BARABARA NA MKUU WA MKOA WA TANGA LUTEN CHIKU GALLAWA WAKIFUATILIA KWA MAKINI HOJA ZA KIKAO HICHO 

Friday, November 25, 2011

MWENGE WAKIMBIZWA TANGA KISHA WAKABIDHIWA MOROGORO

MKUU WA MKOA WA KUSINI PEMBA (aliyeshika Mwenge), MEJA (mstaafu) JUMA K TINDWA AKIMKABIDHI MWENYE WA UHURU MKUU WA MKOA WA TANGA LUTENI (mstaafu) CHIKU GALLAWA MARA BAADA YA MWENGE HUO KUWASILI KATIKA UWANJA WA NDEGE UKITOKEA KISIWANI PEMBA.

MKUU WA MKOA WA TANGA LUTENI (mstaafu) CHIKU GALLAWA AKIWA TAYARI AMEUPOKEA MWENGE WA UHURU KUTOKA KWA MKUU WA MKOA WA KUSINI PEMBA, MEJA (mstaafu) JUMA TINDWA, ANAYEWATAZAMA NI MMOJA WA WAKIMBIZA MWENGE BW. DEOGRATIUS BULLAYI DAFI.

MKUU WA WILAYA YA KOROGWE BW. ERASTO SIMA AKIPOKEA MWENGE WA UHURU KWA HESHIMA BAADA YA MKUU WA MKOA WA TANGA KUSOMA TAARIFA YAKE YA NAMNA MWENGE HUO UTAKAVYOKIMBIZWA KATIKA WILAYA ZA TANGA MJINI NA KILINDI, WA KWANZA KULIA NI MKUU WA WILAYA YA MKINGA BW. RASHID NDAILE.

WAJUMBE WA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YA MKOA WA TANGA WAKISHUHUDIA TUKIO LA KUKABIDHIWA MWENGE WA UHURU MWAKA HUU MKOANI TANGA AMBAO NI MAALUM KWA AJILI YA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA UHURU

MKUU WA MKOA WA MOROGORO BW. JOEL BENDERA AKIWA AMEUPOKEA MWENGE WA UHURU KUTOKA KWA KAIMU MKUU WA MKOA WA TANGA KAMPTENI (mstaafu) SEIF MPEMBENWE ALIYEUKABIDHI MWENGE HUO MKOANI HUMO KWA NIABA YA MKUU WA MKOA WA TANGA ALIYEKUWA NA MAJUKUMU MENGINE YA KITAIFA.

Tuesday, November 15, 2011

WANANCHI TANGA WATOA RAMBIRAMBI KWA WALIOKUFA KWA AJLI YA MELI YA MV SPICE ISLENDARS

MKUU WA MKOA WA TANGA LUTENI (MSTAAFU) CHIKU GALLAWA AKIMKABIDHI MAKAMU WA PILI WA RAIS WA SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR BALOZI SEIF ALLI IDD HUNDI YA SHILINGI MILIONI 11.2 KAMA MCHANGO WA RAMBIRAMBI KWA WANANCHI WA ZANZIBAR KUFUATIA KUZAMA KWA MELI YA MV. SPICE ISLANDERS ILIYOZAMA MIEZI MIWILI ILIYOPITA.
Na Mashaka Mhando,Zanzibar
MKUU wa mkoa wa Tanga, luteni (mstaafu) Chiku Gallawa, amesema wananchi wa mkoa huo, waliupokea kwa masikitiko makubwa msiba wa wananchi waliokuwemo kwenye meli ya Mv Spice Islanders iliyozama miezi miwili iliyopita kwenye mkondo wa Nungwi Visiwani humo, na kwamba wameguswa hasa kutokana na ukaribu wake na visiwa hivyo.

Akizungumza juzi wakati wa kukabidhi rambirambi ya michango kwa ajili ya watu waliopeza maisha kwa Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi, Seif Alli Idd, Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa wanachi wa mkoa wa Tanga waliuopokea kwa masikitiko makubwa msiba huu mzito kutokana na mkoa huo kuwa na mahusiano ya karibu kutokana na kutenganishwa na bahari ya Hindi.

Alisema kuwa msiba huo utazidi kuwaunganisha wananchi wa mkoa huo na Visiwani humo katika kipindi chote cha raha, tabu na majonzi ya kuwakumbuka ndugu zao waliopoteza maisha kwenye jali hiyo na kwamba wataendelea kuwaombea ili mwenyezi Mungu awalale mahali pema peponi.

"Tanga na Zanzibar ni karibu sana na wanachi wa pande zote mbili wana mahusiano ya karibu sana.wameguswa na msiba huu na wameomba tuwasilishe pole nyingi sana pamoja na rambirambi hii ya hundi ya sh 11,288,250, msiba huu utazidi kuwaunganisha katika kipindi chote cha raha na taabu, wameomba mwenyezi mungu aziweke mahali pema peponi roho za marehemu," alisema Mkuu huyo wa mkoa.

Luteni Gallawa aliwataka wale waliokabidhiwa dhima ya kusafirisha abiria katika vyombo vya usafiri wawe wanajali maisha ya watumiaji wao na kwamba wakati mwingine majanga ya namna hiyo yamekuwa yakiepukika lakini kutokana na wasafiishaji kujaza watu kupita kiasi hupelekea matatizo ambayo husababisha maafa kama yaliyotokea kwenye meli hiyo.

Kwa upande wake Makamu wa rais, alishukuru mchango huo kutoka kwa majirani zao wa karibu na kwamba rambirambi hiyo ni kielelezo tosha cha Muungano uliotukuka baina ya wananchi wa visiwani na bara kwa kujaliana katika shida na raha hasa katika ajali hiyo ambayo haiwezi kusauliwa kutoka na uwingi wa vifo vya watu waliopoteza maisha.

"Ulikuwa ni msiba mkubwa katika historia ya Zanzibar, watu 203 walithibitika kufariki na 619 waliokolewa, serkali zote mbili ya Muungano na ya Mapinduzi Zanzibar zilishirikana katika kipidi chote cha janga hili, na kuwasaidia wahanga hao," alisema Makamu huyo wa Rais.

Alisema tume imeundwa kuchunguza mkasa huu na serikali ya SMZ itatoa majibu yake hadharani kwa wananchi ili kuepusha janga kama hilo lisitokee tena na kwamba michango yote itapokelewa na kutumiwa kwa makusudi kwa kadri itakavoamriwa na serikali.

Ujumbe wa Tanga kwenda visiwani humo uliongozwa na Mkuu huyo wa mkoa, pia walikuwemo Mwenyekiti wa CCM mkoa Bw. Mussa Shekimweri Mkuu wa wilaya ya Tanga Dkt Ibrahim Msengi, Mkuu wa wilaya ya Muheza Bw. Methew Nasei na mwakilishi wa wafanyabiashara mkoani Tanga Bw.Salim Abdallaziz  kutoka kampuni ya unga wa ngano ya Pembe.

Sunday, November 6, 2011

KUMBE KUNA SAMAKI WAKUBWA KIASI HIKI!

VIJANA WA KIJIJI CHA BAGAMOYO KILICHOPO WILAYANI KOROGWE WAKIVUA SAMAKI KATIKA DARAJA MOJA WAPO AMBALO LINAJENGWA NA KAMPUNI YA KICHINA YA SINOHYDRO, DARAJA HILO LIPO JIRANI NA MTO PANGANI AMBAO MAJI YA MTO HUO YAMEKATISHA BARABARA HIYO NA VIJANA HAO KUPATA NAFASI YA KUVUA SAMAKI

JUMA (KUSHOTO) NA SUFIANI WAKIVUA SAMAKI

ADAM NA SAID WAKIVUA SAMAKI KWA CHANDARUA KILICHOTOLEWA KWA AJILI YA KUJIKINGA NA MALARIA, LAKINI WANAKITUMIA KUVULIA SAMAKI.

VIJANA WAKIVUA HUKU WAKICHEZA KATIKA DARAJA HILO

SAMAKI WALIOVULIWA KATIKA DARAJA HILO

"...TUNAPATA SAMAKI HAPA, WEEE USICHEZE SI UNAWAONA HAWA...SHULE KWANINI BANA SI NAVUA NIKIUZA NITAPATA PESA...,ANASEMA GUMBO MLIMBO

Wednesday, November 2, 2011

TICTS YAKUTANA NA WADAU WAKE KWENYE HOTELI YA TANGA BEACH RESORT

OFISA MTENDAJI MKUU WA TICTS BW. NEVILLE BISSETT AKIELEZEA NAMNA KAMPUNI HIYO YA KUPAKUA MAKONTENA KATIKA BANDARI YA DAR ES SALAAM JINSI ITAKAVYOWEZA KUONGOZA KATIKA KAZI YA KUPAKUA MAKONTENA KATIKA NCHI ZA KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA.

WADAU WA MKUTANO ULIOITISHWA NA TICTS KWENYE HOTELI YA TANGA BEACH RESORT KUZUNGUMZIA CHANGAMOTO ZA KAMPUNI HIZO.

WADAU WAKISIKILIZA KWA MAKINI MKUTANO WA WADAU WA TICTS

WADAU WAKIPIA PICHA YA PAMOJA KWENYE HOTELI YA TANGA BEACH RESORT JIJINI TANGA.