Blogu hii imedhaminiwa na Simba Video Coach

Blogu hii imedhaminiwa na Simba Video Coach
Kwa usafiri wa Dar es salaam, Morogoro, Dodoma na Arusha, safiri kwa raha na Simba Mtoto Luxury Coach

Sunday, July 31, 2011

YANGA YAIKACHA COASTAL LEO KUOGOPA MAKWANJA

MABINGWA WA SOKA TANZANIA BARA, YANGA SPORTS CLUB WAMEINGIA MITINI KWA KUAHIRISHA MCHEZO WAO WA KIRAFIKI DHIDI YA 'WAGOSI WA KAYA' COASTAL UNION AMBAYO KWA SASA IPO FITI ASILIMIA 90 KUKABILIANA NA MIKIMIKI YA LIGI KUU YA VODACOM ITAKAYOANZA MWEZI UJAYO. YANGA WAMEAAHIRISHA MECHI HIYO WAKIELEZA KWAMBA KUCHEZA MCHEZO HUO KUTAVURUGA MAANDALIZI YAO YA MCHEZO WA NGAO YA HISANI HAPO AGOSTI 17 MWAKA HUU WATAKAPOCHEZA NA WAPINZANI WAO WAKUBWA SIMBA. HATA HIVYO HABARI ZILIZOZAGAA KATKA MITAA YA NGAMIANI ZINASEMA YANGA WAMEUKACHA MCHEZO HUO ULIOKUWA UPIGWE LEO KWENYE UWANJA WA CCM MKWAKWANI, KUTOKANA NA KUAMINI KWAMBA COASTAL NA SIMBA NI KITU KIMOJA HIVYO WACHEZAJI WA COASTAL WANAWEZA KUTUMIWA NA UONGOZI WA SIMBA KUWAAMUMIZA WACHEZAJI WAO ILI WASHINDWE KUCHEZA VYEMA SIKU HIYO YA NGAO YA HISANI, MANENO HAYO!!! 

HATIMAYE UBINGWA WA POOL WATOKA DAR WAENDA DODOMA

MBUNGE WA KIBAKWE MH. GEORGE SIMBACHAWENE (kulia) AMBAYE ALIKUWA MGENI RASMI KATIKA FAINALI YA MASHINDANO YA SAFARI LAGER NATIONAL POOL CHAMPIONSHIRP MJINI DODOMA, AKIMKABIDHI MMOJA WA VIONGOZI WA MKOA WA DODOMA AMBAO WAMEKUWA MABIGWA WA MWAKA 2011

MGENI RASMI MH. GEORGE SIMBACHAWENE (MP) WA KIBAKWE AKIMKABIDHI KITITA CHA SH. MILIONI 5 KWA NAHODHA WA TIMU YA POOL YA MKOA WA DODOMA AMBAYO IMETWAA UBINGWA MWAKA HUU BAADA YA KUIFUNGA KINONDONI AMBAO NI MABIGWA WA MWAKA JANA, UBINGWA WALIOUTWAA JIJINI ARUSHA.

MWENYEKITI WA POOL TAIFA BW. ISAACK TCHOGOSHO AKIMKABIDH KITITA CHA SHILINGI MILIONI KIONGOZI WA MKOA WA MWANZA AMBAO WAMETWAA USHINDI WA TATU KATKA MASHINDANO HAYO.

MABINGWA WAPYA WA MASHINDANO YA SAFARI LAGER NATIONAL POOL CHAMPIONSHIRP MKOA WA DODOMA.

Saturday, July 30, 2011

BILION 121 ZAHITAJIKA KUKARABATI MRADI WA MAJI WA HTM HANDENI

ADAM MGANGA MPIGA NGOMA YA UFUNGILO AKIASHIRIA KUANZA KWA BARAZA LA MADIWANI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA HANDENI, JULY 28 MWAKA HUU.

WAHESHIMIWA MADIWANI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA HANDENI WAKIWA KATIKA MKUTANO WAO WA BARAZA LA MADIWANI (FULL-COUNCIAL) WILAYANI HANDENI.

WAGENI WAALIKWA, WATENDAJI NA WAANDISHI WA HABARI WAKIFUATILIA KIKAO HICHO AMBACHO PAMOJA NA MAMBO MENGINE WALIZUNGUMZIA SUALA LA UKOSEFU WA MAJI KATKA WILAYA HIYO AMBAPO MENEJA WA MRADI WA MAJI WA HTM INJINIA ALEX MSILANGA ALISEMA MRADI HUO UNAHITAJI KIASI CHA SHILINGI BILIONI 121 UKARABATI WAKE ILI KUTATUA TATZO LA MAJI HANDENI.

MADIWANI WAKIFUATILIA MKUTANO HUO WA BARAZA LA MADIWANI NA KUCHANGIA HOJA MBALIMBALI.

MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA HANDENI BW. HASSAIN MWACHIBUZI (kulia), MWENYEKITI WA HALMASHAURI HIYO BW. RAMADHANI DILIWA NA KULIA KWAKE NI MAKAMO WAKE.

NGOMA YA UFUNGILO HANDENI

ADAM ATHUMANI MGANGA MPIGA NGOMA YA UFUNGILO INAYOASHIRIA KUANZA KWA BARAZA LA MADIWANI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA HANDENI, MGANGA ALIANZA KUPIGA NGOMA HII TANGU MWAKA 1979 HADI SASA BAADA YA KUIRITHI KUTOKA KWA MZEE JUMA KIGWADUKE.

Tuesday, July 26, 2011

KAZI YA BWANA AFYA WA JIJI AIFANYA KALEMBO, UWASA HARAKA WAUZIBUA MFEREJI ULIOKUWA UKITIRIRISHA MAJI BARABARANI

MKUU WA MKOA WA TANGA MEJA JENERALI SAIDI KALEMBO AKIANGALIA NAMNA JIJI WASIVYOWEZA KUZIBUA MITARO AMBAYO INAWEZA KULETA MAGONJWA YA MILIPUKO. HAPA NI SEHEMU YA HOTELI YA SALZ NYUMA YA HOTELI YA SP JIRANI KABISA NA MLANGO WA KUINGILIA HALMASHAURI YA JIJI LA TANGA.

KALEMBO ATEMBELEA MFEREJI AFRITEX (CIC) UNAOMWAGA KEMIKALI ZA SUMU

MWENYEKITI WA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA MKOANI TANGA, MEJA JENERALI SAID KALEMBO (MWENYE TAI KATIKATI YA PICHA) AKIONYESHWA MFEREJI MAMA WA JIJI AMBAO HUANZIA KWENYE KIWANDA CHA AFRITEX NA KUTITIRISHA MAJI YANAYODAIWA KUWA NA KEMIKALI ZA SUMU.



Na Mwandishi Wetu,Tanga
MKUU wa mkoa wa Tanga Meja Jererali (Mstaafu), Said Kalembo ameuagiza uongozi wa Jiji la Tanga kuchukua hatua za haraka juu ya tatizo la viwanda vinavyotiririsha maji yenye kemikali na kusababsiha madhara kwa binadamu katika mfereji mama unaopita kata sita za Jiji hilo  kwenda baharini, unapatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Akizungumza juzi wakati mkuu huyo na Kamati yake ya Ulinzi na Usalama ya mkoa walipotembelea mfereji huo kuona namna maji yanayodaiwa kuwa na kemikali yakimwagwa kutoka viwandani na kuleta athari kwa binadamu na viumbe wengine wanaotumia mfereji huo kuufanyia usafi.

Awali Ofisa Afya wa Jiji hilo, Yusuph Gumbo akimsomea taarifa mwenyekiti huyo wa Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa, alisema kuwa Julai 11 mwaka huu vibarua 14 waliokuwa wakifanya usafi kwenye mfereji huo kwa kuingia katikati, walipata madhara makubwa ya kuungua miguuni kwa kubabuka ngozi baada ya kuingiwa na maji yanayodhaniwa kuwa kemikali zenye sumu.

Alisema vibarua hao walipokuwa wakisafisha mfereji huo wenye urefu wa kilomita nane, licha ya kuvaa viatu virefu (Gum Boots) hata hivyo maji ya mfereji huo yaliwaingia na kujisikia kuwashwa baada ya muda wa masaa mawili walipotoka katika mfejei huo na kisha kuanza kubabuka na hali zao kuwa mbaya.

“Kwa vile vibarua wale walikuwa wakipokezana kuingia ndani ya mfereji  waliamua kutoka ili wenzao wengine waingie waendelee na usafi, lakini wale waliotoka mferejini baada ya kuvua viatu muwasho ulizidi na mmoja kati yao ambaye aliungua vibaya na ngozi ilibabuka na kufanya awe na vidonda kuanzia magotini hadi miguuni,” alisema Gumbo.

Aliongeza kwamba mfereji huo uliojengwa miaka ya 1970 kwa ajili ya kusaidia kutoa maji ya mvua na kuyapeleka maharini lakini sasa umekuwa ukitumiwa na viwanda kumwaga mabaki ya takataka zao na kuvitaja viwanda hivyo kuwa ni kiwanda cha nguo cha Afritex, Kiwanda cha kusindika samaki cha Sea Food Products, Kiwanda cha foma, Kiwanda cha Vioo (Tansilica), karakana ya Tanroads na karakana za magari zilizopo eneo la viwanda Gofu.

Hata hivyo, alisema hatua ambazo halmashauri ya jiji imechukua hadi sasa ni kuwapa notisi ya kisheria wenye viwanda hivyo na kuwataka kuwa na mitambo ya kusafishia majitaka wanayoyatiririsha kabla ya kumwagwa baharini na kiwanda cha Afritex tayari kimenunua mtambo huo lakini bado haujaanza kusafisha maji hayo.

Mwana mazingira wa Envirocare Haika mcharo ambaye ni ofisa habari wa taasisi hiyo inayojihusisha na suala la mazingira hapa nchini, alimweleza Mkuu wa huyo wa mkoa katika ziara hiyo kwamba serikali inatakiwa kuchukua hatua juu ya tatizo hilo kwa ajili ya kulinda viumbe hai vya baharini na binadamu na wananchi wanaoishi pembezoni mwa mfereji huo.

“Mheshimiwa Mkuu wa mkoa kabla ya kufanya ziara hapa na kamati yako, juzi (Alhamisi) nilitembelea kiwanda cha Afritex nikiwa na waandishi wa habari kuona namna kiwanda hiki kinavyojiendesha hasa sual la mazingira tumeona maji yao wanayoyatitiisha lakini tunadhani wakati mwingine maji yanakuja kwenye mfereji huu bila kusafisha, ni vema serikali ya mkoa ikatilia mkazo suala hili mapema kabla ya athari kubwa haijapatikana,” alisema mcharo.

Kufuatia hali hiyo Mkuu wa mkoa alimwagiza viongozi wa Jiji pamoja na Mkuu wa wilaya ya Tanga Dkt Ibrahim Msengi kuhakikisha wanachukua hatua za haraka ikiwezekana kuvifungia viwanda walivyobainika kumwaga kemikali hizo zenye sumu kwani tayari madhara kiafya yamepaikana kwa vibarua hao waliobabuka ngozi kuliko kukaa na kulalamikia suala hilo.
MWISHO

MSHIKE MSHIKE WA KUDAKA ABIRIA STENDI YA TANGA

WAPIGA DEBE STENDI YA TANGA WAKIMNG'ANG'ANIA ABIRIA (DADA ALIYEKUWA NA KIPOCHI MWENYE ALIYEVAA SURUALI NYEUSI) KUPANDA KWENYE MABASI YAO KILA MMOJA AKITAKA KUMKATIA TIKETI YA KWENDA MOROGORO LEO ASUBUHI.

Sunday, July 24, 2011

KAMANDA MPYA WA POLISI TANGA AANZA KAZI KWA KUKAMATA SMG NA BASTOLA

KAMANDA MPYA WA POLISI MKOANI TANGA ACP CONSANTINE MASAWE AKIWAONYESHA SILAHA WALIZOKAMATA HUKO MTONI BOMBO WILAYANI KOROGWE BAADA YA KUMKAMATA JAMBAZI SUGU

KAMANDA MPYA WA POLISI MKOANI TANGA ACP CONSTANTINE MASAWE AKIJARIBU KUIPIGA SILAHA AINA YA SMG WALIYOIKAMATA KWA JAMBAZI MMOJA HUKO KOROGWE

BAADHI YA WAANDISHI WA HABARI WALIOFIKA KWENYE OFISI YA KAMANDA MPYA WA POLISI MKOANI TANGA KUKUTANA NAYE KWA MARA YA KWANZA AMBAPO ALIWAPA HABARI YA KUKAMATA BUNDUKI AINA YA SMG NA BASTOLA (KULIA) NI WILLIAM MNGAZIJA AKIMSIKILIZA KWA MAKINI KAMANDA HUYO (KUSHOTO).

PROFESA J AWARUSHA WANAFUNZI ONESHO LA MALARIA HAIKUBALIKI

WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI USAGARA WAKIFUATILIA KWA MAKINI ONESHO LA KAMPENI YA KUPIGA VITA MALARIA HAIKUBALIKI LIKIONGOZWA NA WASANII WA THT AKIWEMO PROFESA J AMBAYE ALITOA BURUDANI ILIYOFURAHIWA NA WANAFUNZI WENGI WALIOHUDHURIA.

PROFESA J AKITOA BURUDANI KWENYE UWANJA WA SHULE YA SEKONDARI YA USAGARA SEKONDARI JIJINI HAPA AKISHIRIKIANA KUIMBA NA MWANAFUNZI MMOJA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA MOJA LA ZENNA WIMBO WA 'ZARI LA MENTALI' KIBAO AMBACHO KWA HAKIKA KILIWABURUDISHA IPASAVYO WANAFUNZI.

PROFESA J AKIIMBA PAMOJA NA MMOJA WA WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI GALANOSI AMBAYE ALIKUWA AKISHINDANA NAYE KUIMBA KIBAO 
 MCHANGANYIKO.
Professor Jay and Ditto meet with studnets in Tanga using performance to fight malaria
July 21st 2011.
On the 21stof July, students from ten schools came together at Usagara Secondary School in Tanga town to take part in malaria themed song, theatre and poetry competitions. The competition was a part of the Zinduka! club initiative, in which youth are empowered with the knowledge and tools to drive forward the fight against malaria in local communities. The judges were treated to a spectacle of talent as they witnessed an array of performances including poetry readings, songs and even theatrical performances
On reaching the final round, Tanzanian artist, Ditto, took to the stage to talk to the students about how important it is to protect themselves from malaria to ensure they secure their future, before the artist sang the malaria he had written for the Zinduka! campaign which has now become an anthem for a generation fighting against malaria.
The students were then surprised when another guest Bongo fleva rapper and Zinduka! goodwill ambassador Professor Jay joined Ditto on stage to sing the anthem. The artist has been a prominent figure in the fight against malaria, featuring in the launch of the Zinduka! campaign in 2010 and making regular appearances for the campaign in the field and on TV.Professor Jay then took time to hand out awards to the lucky competition winners.
Professor J had this to say, “I joined the Zinduka! campaign with the hope that through my music I could help to fight malaria in Tanzania. But to see kids wanting to get involved and using music as the platform to fight malaria in their communities, that’s what makes me most proud of the work we have done.
Professor Jay and Ditto then invited youth to join him as he visited a number of houses near Tanga town, where the youth spoke to households about what measures they use to protect themselves from malaria and what they think needs to be done to eradicate malaria in Tanzania.

The Malaria Haikubaliki Campaign is led by the Tanzanian Government behind the leadership of President JakayaKikwete. It is supported by partners including Malaria No More, Tanzania House of Talent (THT), Johns Hopkins University, Population Services International and United Against Malaria. The goal of the program is to achieve universal bed net coverage and eliminate malaria deaths by urging all Tanzanians to Zinduka! (“Wake up!”) to the threat of malaria and protect themselves against the disease.


 
              











Friday, July 15, 2011

SIMBA VIDEO COACH YATOA MABASI MAPYA

KWA USAFIRI WA RAHA SAFIRI NA BUS LA SIMBA VIDEO COACH KWA SAFARI ZAKO ZA DAR ES SALAAM, DODOMA, MOROGORO NA ARUSHA

BUS JIPYA LA SIMBA VIDEO COACH LINAVYOONEKANA KWA NDANI

Wednesday, July 13, 2011

DC ACHELEWA BAADA YA GARI LAKE KUHARIBIKA

Katibu Tawala (DAS) wa wilaya ya Korogwe Mr Kembo aliyevaa suti (kulia) akisisistiza gari litengenezwe haraka ili Mkuu wa wilaya ya Korogwe Bw. Erasto Sima awezekusafiria gari hilo ambalo lilikuwa haliwaki wakati akitaka kwenda vijijini kwa kazi za maendeleo

Tuesday, July 12, 2011

SHEREHE ZA IDADI YA WATU DUNIANI ZAFANA MUHEZA

Mkuu wa mkoa wa Tanga, Meja Jenerali (mstaafu) Said Kalembo akisoma hotuba yake kwenye sherehe za kitaifa za maadhimisho ya siku ya idadi ya watu duniani iliyoadhimishwa kwenye uwanja wa Jitegemee wilayani Muheza ilikofanyika Kitaifa hapa nchini,kulia kwa Bw. Kalembo ni Waziri wa Fedha, uchumi na Mpango wa Maendeleo wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar Bw. Omar Yusuph Mzee, kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wilayani Muheza Bw. Peter Jambele.

Maofisa wa kamati ya ulinzi na usalama kutoka kushoto Kaimu RPC Tanga Mohamed Jafar, mwakilishi wa ofisi ya RSO mkoani Tanga, Mwakilishi wa magereza wakifuatilia kwa makini sherehe hizo.

Mkuu wa mkoa meja jenerali Said kalembo pamoja na waziri wa fedha, uchumi na mpango wa maendeleo wa serikali ya mapinduzi zanzibar Bw. Omar yusuph mzee wakiwa katika picha ya pamoja na wakurugenzi wa halmashauri za wilaya za Tanga pamoja na wenyeviti wa halmsauri hizo mara baada ya Mkuu wa mkoa kusoma hutuba kwenye sherehe za maadhimisho ya siku ya idadi ya watu duniani iliyofanyika kitaifa wilaya ni Muheza.

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Pangani Bw. Salim Sinani (kushoto) akiteta jambo na Meya wa Jiji la Tanga Bw. Omar Guled kwenye sherehe za idadi ya watu duniani zilizofanyika wilayani Muheza.

Saturday, July 2, 2011

COASTAL UNION YAPATA UONGOZI MPYA

VIONGOZI WAPYA WA KLABU YA COASTAL UNION WALIOCHAGULIWA LEO MAKAO MAKUU YA KLABU HIYO BARAARA 11 JIJINI TANGA, KUTOKA KUSHOTO NI ALBERT PETER (Mjumbe), SALIM AMIR (Mjumbe), AHMED HILAL 'AURORA' (Mwenyekiti), JAMES MWINCHANDE (Mjumbe) NA JULIUS BENJAMIN MJUMBE PIA MARA BAADA YA KUCHAGULIWA KWENYE MKUTANO MKUU WA UCHAGUZI.

MWENYEKITI MPYA WA KLABU YA COASTAL UNION (kushoto) AKIVALISHWA KITAMBAA CHEKUNDU NA MMOJA YA WANACHAMA WA SIKU NYINGI WA KLABU HIYO MICHENI AHMED MICHENI BAADA YA KUTANGAZWA KUWA MSHINDI KISHA MWANACHAMA HUYO KUMPONGEZA KWA KUMVIKA KITAMBAA HICHO.

WANACHAMA WAKIWA TULI WAKIFUATILIA KWA MAKINI MATOKEO YA UCHAGUZI YAKITANGAZWA NA MWENYEKITI WA UCHAGUZI WA KLABU HIYO ABDALLAH YAHYA (hayupo pichani) WAKATI WA KUHESABU KURA ZILIZOPIGWA NA WAJUMBE WALIOFIKA KWENYE UCHAGUZI HUO.

WANACHAMA WA KLABU YA COASTAL UNION WAKIFUATILIA KWA MAKINI ZOEZI ZIMA LA UCHAGUZI LILILOVYOKUWA LIKIENDESHWA KATIKA KLABU HIYO HATUA AMBAYO IMEWEKA HISTORIA YA KLABU HIYO KUFANYA UCHAGUZI MKUU WA VIONGOZI WAKE BAADA YA MIAKA TISA TANGU ULIPOFANYIKA UCHAGUZI WA KIKATIBA MWAKA 2002.

MCHEZAJI WA SIKU NYINGI WA KLABU YA YANGA KITWANA MANARA (aliyesimama) AKITOA NASAHA ZAKE KAMA MMOJA YA VIONGOZI WA KAMATI YA UCHAGUZI WA SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI TFF AKIELEZEA TARATIBU ZILIZOSABABISHA HADI KLABU HIYO IKAFANYA UCHAGUZI WAKE HUO WA VIONGOZI.

MWENYEKITI MPYA WA KLABU YA COASTAL UNION AHMED HILAL 'AURORA' (wa pili kushoto) AKIWA NA WAJUMBE WAKE NA BAADHI YA WANACHAMA AKIWEMO KITWANA MANARA (kushoto kwake), STEVEN MGHUTO, ALBERT PETER NA MWENYE KANZU NI ALYEKUWA MWENYEKITI WA KLABU HIYO KAMATI YA MUDA MZEE TALHATA
Na Mashaka Mhando,Tanga
KLABU ya Coastal Union ya Jijini Tanga, leo imefanya uchaguzi wake wa kikatiba wa kuchagua viongozi wake watakaoiongoza klabu hiyo kwa kipindi cha muda wa miaka mitatu baada ya miaka takribani taisa kuongozwa na kamati za muda.

waliochaguliwakatika mkutano huo ambao awali ulikuwa ufanyike wiki iliyopita lakini ulisimamishwa na TFF (shirikisho la soka nchini) baada ya kuwaengua wagombea saba ambao hawakuwa na sifa za kuwania nafasi hizo ni pamoja na Mwenyekiti Ahmed Hilal 'Aurora' ambaye hakuwa na mpinzani baada ya kujizolea kura 52 kati ya wajumbe 55 waliojitokeza kushiriki uchaguzi huo.

Wajumbe waliochaguliwa kura zao zikiwa kwenye mabano ni pamoja na Kweli Nahashon (48), Albert Peter (47), Salim Amir (42), Julius Benjamin (42) na James Mwinchande ambaye alipata kura 36.

Akitangaza matokeo hayo msimamizi wa kamati ya uchaguzi wa klabu hiyo Abdallah Yahya alisema kuwa watu waliojiandikisha kupiga kura kwa maana wanachama halali walikuwa 77 lakini kwenye uchaguzi huo wamefika wanachama 55 hivyo uchaguzi huo ulifanyika kutokana na koram ya wajumbe kutimia.

Alisema kwa mujibu wa katiba ya Coastal Union viongozi wanatakiwa kuwa tisa kwa maana Mwenyekiti, Makamo Mwenyeki na wajumbe saba lakini kutokana na kwamba kumebaki nafasi tatu za makamo mwenyekiti na wajumbe wa tatu uchaguzi mwingine utaitisha mara baada ya wanachama ambao walienguliwa kukamilisha taratibu za kuwasilisha vyeti wakikamilisha.

Wanachama ambao waliomba lakini walienguliwa ni pamoja na Makamo Mwenyekiti Steven Mghuto na Titus Bandawe, Yakob Nuru, Jawa Bakari Jawa, Ayub Athumani na Kilo Rashid.

Kwa mara ya mwisho klabu hiyo ilifanya uchaguzi wake wa kikatiba mwaka 2002 ambapo marehemu Zacharia Kinanda 'Arrigo Sacchi' aliachaguliwa kuwa Katibu Mkuu na wakati huo huo akiwa kocha mkuu wa timu hiyo na Mbwana Abushiri 'Director' akiwa mwenyekiti.
MWISHO

MASIKINI BANDARI YA TANGA HIVI NI KWELI WAFANYABIASHARA HAWAPENDI KUITUMIA SABABU YA TRA?

BANDARI YA TANGA INAVYOONEKANA PICHANI

BANDA LINALOFANYA BIASHARA YA MNADA WA SAMAKI LILILOPO ENEO LA DEEP SEA KATIKA JIJI LA TANGA NI MOJA YA ENEO LA SIKU NYINGI SANA PEMBEZONI MWA BANDARI YA TANGA.

SHAZI HILI LA SAMAKI LILIUZWA SH. 18,000, SAMAKI SASA HIVI WANABEI SANA NA HASA HII JULAI!

WADAU WATAKA TAMASHA LA FILAMU TANGAMANO LIFANYIKE KILA MWAKA

TAMASHA la wazi la sinema ambalo linafikia kelele chake leo kwenye uwanja wa Tangamano huku filamu iliyoongozwa na Single Mtambalike (Richie) na kuzalishwa na Suleiman Said Barafu ya Senior Bachelor ndiyo iliyofunga pazia la tamasha hilo huku wadau wa filamu wakiomba tamasha hilo lifanyike kila mwaka mjini hapa.

Tamasha hilo ambalo lilikuwa la wiki moja ambalo limedhaminiwa na Grand Malt Tanzania lilianza Juni 27 katika viwanja ya Tangamano Mjini Tanga, lilihudhuriwa na maelfu wa Jiji la Tanga na wilaya jirani ambao wameweza kuwaona wasanii waliokuwa wakiwaona tu luningani.

Filamu hiyo ambayo ilioneshwa kwenye uwanja huo ilitanguliwa na maelezo kutoka kwa muigizaji wake Jacob Steven maarufu kama JB ambaye ameshajizolea umaarufu mkubwa kupitia filamu kadha alizoigiza. 
 
 
 

FAX JAZZ INAVYOKONGA NYOYO ZA WATU TANGA HOTEL

WANA-MUZIKI WA BENDI MAARUFU JIJINI TANGA YA FAX JAZZ BAND AMBAYO IMEKUWA IKITUMBIZA KILA SIKU ZA ALHAMISI, IJUMAA, JUMAMOSI NA JUMAPILI KATIKA UKUMBI TANGA HOTELI AMBAKO MASHABIKI MBALIMBALI WA MUZIKI WA DANSI WAMEKUWA WAKIFURIKA. PICHANI NI MWIMBAJI KIDUCHU AKIWA NA MGOSIGWA AKIKUNG'UTA GITAA LA RYTHIM.

MSHABIKI MAARUFU WA MUZIKI UNAOAPIGWA TANGA HOTEL MR RASTA AKISAKATA MUZIKI WA FAX AKIWA NA MKEWE KWENYE UKUMBI HUO WA TANGA HOTEL.

MRATIBU WA UKIMWI WA JIJI LA TANGA MR MOSES NAYE HAKUBAKI NYUMA ALIKUTWA NA KAMERA YETU AKISAKATA MUZIKI WA FAX HUKU AKIMWAGA SERA ZA UPIMAJI WA HIARI WA VIRUSI VYA UGONJWA FAKIRI WA UKIWMI.

SHIRIKA LA SAHiRNGON YAJIKITA MUHEZA KUFUNDISHA NAMNA YA UFUATILIAJI WA FEDHA ZA KILIMO ZINAZOTUMWA NA SERIKALI WILAYANI HUMO

MRATIBU WA MTANDAO WA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YA HAKI ZA BINADAMU KUSINI MWA AFRIKA (SAHiRNGON) MARTINA  KABISAMA (wa kwanza kushoto) AKIWA PAMOJA NA VIONGOZI MBALIMBALI WA WILAYA YA MUHEZA MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MUHEZA KIROBOTO, ALEX MBEJO KWENYE MKUTANO WA WADAU WA KUFUATILIA FEDHA ZA KILIMO NA MIFUGO WILAYANI HUMO.

MRATIBU WA SHIRIKA LA SAHiRNGON MARTINA KABISAMA AKIZUNGUMZA NA WAJUMBE WA KAMATI ZA KUFUATILIA FEDHA ZA KILIMO WILAYANI MUHEZA KUTOKA KATA ZA TONGWE, KISIWANI NA NKHUMBA KWENYE MKUTANO ULIOFANYIKA KWENYE HOTELI YA AMBASSADOR WILAYANI HUMO.

WAJUMBE WA KAMATI ZA UFUATILIAJI WA FEDHA ZILIZOLETWA NA SERIKALI KWA AJILI YA KILIMO WILAYANI MUHEZA KUTOKA KATA ZA TONGWE, KISWANI NA KHUMBA WAKIMSIKILIZA MRATIBU WA SHIRIKA LA SAHiRNGON MARTINA KABISAMA (hayupo pichani) KWENYE MKUTANO ULIOFANYIKA WILAYANI MUHEZA.

SI KWAMBA WAMECHOKA AU WANASINZIA KUTOKANA NA UCHOVU WA KUKAA MUDA MWINGI LA HASHA! BALI WAJUMBE HAWA KUTOKA KATA ZA TONGWE, KISIWANI NA NKHUMBA WAKISIKILIZA KWA MAKINI NAMNA SERIKALI INAVYOWEZA KUTUMA FEDHA VIJIJINI NA WAKATI MWINGINE FEDHA HIZO HAZIONEKANI NA WALA HAZITUMIKI KWA MIRADI ILIYOKUSUDIWA HIVYO WAJUMBE HAO WAKAONEKANA HAWAELEWI UTARATIBU UNAVYOTUMIKA KUJUA FEDHA HIZO ZINAWEZEKANAJE KUFIKA BILA KUTUMIWA.

Friday, July 1, 2011

MASHINDANO YA POOL MKOANI TANGA KUANZA SPLENDID NA MAGROVE JULY 7 HADI 10 KWA VILABU VINANE KUCHUANA

MSIMU WA MASHINDANO YA KUTAFUTA KLABU BINGWA YA MCHEZO WAPOOL MKOANI TANGA UMEANZA, PICHANI NI MENEJA WA BIA YA SAFARI LAGER MKOANI TANGA MR. MBISE (kushoto) AKIWA NA KATIBU MKUU WA CHAMA CHA POOLTABLE MKOA WA TANGA (TARPA) SHABAN KIBELLOH WAKIWA KATIKA UKUMBI WA HOTELI YA ZE CITY KULIKOKUWA NA 'SPEED POOL'

WATAALAM WA KAMPUNI YA INTERGRETED YA JIJI DAR ES SALAAM INAYOHUSIKA NA MATANGAZO YA BIA YA SAFARI LAGER WAKITOA MATANGAZO YAO KUHUSU KUANZA RASMI KWA MASHINDANO YA POOL MKOANI TANGA.

KATIKA MSIMU HUU WA MASHINDANO YA POOL KULIKUWA NA SHINDANO DOGO LA KUTAFUTA BINGWA ANAYEWEZA KUINGIZA KETE ZOTE 15 NDANI YA DAKIKA 3 TU NA PICHANI NI BINGWA ALIYEWEZA KUINGIZA KETE HIZO KWA KUTUMIA DAKIKA 2 NA SEKUNDE 32 HUYO SI MWINGINE NI ALLY SHARIFF MCHEZAJI WA KLABU YA KWAMINCHI. HII NI SPEED POOL.

HAPA MSHINDI WA SPEED POOL ALLY SHARIFF AKIWA NA MTANGAZAJI WA INTERGRETED BI LATIFA MARA BAADA YA KUKABIDHIWA ZAWADI YAKE KISHA KUVALIA JEZI YAKE YA SAFARI LAGER HAPA AKIONGEA MANENO MAWILI MATATU NA LATIFA.